Saturday, 6 December 2014

USHAURI; Jinsi Ya Kukuza, Kustawisha Na Kuendeleza Biashara


Moja ya changamoto kubwa kwenye biashara nyingi ni jinsi ya kuzikuza na kuendelea zaidi. Kuna biashara nyingi huku mitaani ziko vile vile miaka nenda miaka rudi. Pamoja na kuwepo hivyo hivyo kila mwaka bado wamiliki wa biashara hizi jawajapata mafanikio waliyotegemea kuyapata. Hili limekuwa tatizo kwa watu wengi sana na huenda ni tatizo ambalo limekusumbua wewe muda mrefu.
Kabla ya kuona ni jinsi gani unaweza kukuza, kustawisha na kuendeleza biashara yako naomba tuone alichoandika msomaji mwenzetu wa AMKA MTANZANIA.
Mimi ni mfugaji wa ng'ombe,mbuzi na kondoo pia nina duka la rejareja mwaka wa 3 sasa.Shida yangu ni namna ya kukuza ,kustawisha na kuendeleza biashara hii ya duka hadi kiwango cha kukidhi mahitaji ya wateja wote. Nimeplan mara nyingi kufikisha kiwango fulani cha mauzo mwisho nikifanya tathmini sijafikia ama nimeshuka kiwango.Naomba msaada ni mbinu zip nawezatumia kufikia lengo langu la kuikuza bishara.
Kama alivyosema msomaji mwenzetu hapo juu hii ni kiu ya wafanyabiashara wengi sana, jinsi ya kukuza biashara zetu.
Inawezekana unaweka mipango mizuri ila bado huoni matokeo mazuri. Kuna mambo mengi unaweza kufanya kukabili changamoto hii, hapa nitaeleza mambo manne ambayo unaweza kuanza kufanya na ukaona mabadiliko makubwa.
1. Weka malengo na mipango mizuri ya kufanikiwa.
Huu ndio mwanzo kabisa wa safari ya mafanikio katika jambo lolote unalofanya. Ila pia inawezekana umeshafanya hivi na bado umeshindwa kupata mafanikio. tatizo inakuwa nini?
Tatizo linaweza kuwa unaweka malengo yako vibaya au huweki mipango yako vizuri. Malengo na mipango unayoweka hakikisha inaeleza kwa kina kabisa ni kitu gani utafanya wakati gani na ni marekebisho gani unahitaji kufanya ili uweze kufanikiwa. Kusema tu labda baada ya miezi sita nataka nifikie mauzo ya milioni kumi haitoshi kukufikisha hapo. Ni lazima uchambue ni nini utabadili sasa ili uweze kufikia malengo hayo ya kuuza milioni kumi.
Kuna mambo mengi sana ya kurekebisha kwenye biashara hasa za reja reja ili kuweza kufikia mafanikio makubwa. Mambo kama jinsi unavyofanya biashara, muda unaofungua na kufunga, wafanyakazi unaoajiri, jinsi unavyochangamana na wateja na hata imani yako kwenye biashara yana nafasi kubwa sana kwenye mafanikio ya biashara yako. Hakikisha haya yamekaa vizuri kwanza kabla hujaona mafanikio makubwa kwenye biashara yako.
kitabu kava tangazo
2. Jua ni wapi unakosea na ufanye marekebisho haraka.
Kama unaweka malengo na mipango ila bado unashindwa kuifikia ni dhahiri kuna sehemu unakosea kwenye mipango yako au uteklezaji wa mipango yako. Na ili uweze kujua hilo ni lazima kila unaposhindwa kufikia lengo ujifanyie tathmini ya yote uliyofanya ili kujua ulikosea wapi. Sisi ni binadamu hivyo tunakosea mara nyingi sana, kitu kizuri ni kwamba tunapokosea ndipo tunapojifunza. Tumia makosa yako kama sehemu ya kujifunza ni njia ipi bora kwako kufikia malengo yako.
Sio kila mipango utakayokuwa nayo kwenye biashara yako itakuletea mafanikio. Jipime kila mara na jua ni mipango ipi inaleta mafanikio na ipi haileti mafanikio.
3. Kua wewe kwanza.
Moja ya sababu kubwa kwa nini biashara yako haikui ni kwa sababu wewe mwenyewe hukui. Biashara yako haiwezi kukua kama wewe mwenyewe hukui, sahau kabisa kuhusu hilo. Cha kushangaza asilimia kubwa ya watu wanataka biashara zao zikue wakati wao bado wako vile vile na wanafikiri vile vile, kitu ambacho hakiwezi kutokea. Wewe unakuaje? Unakua kwa kujifunza kuhusu biashara kupitia kujisomea vitabu, makala nzuri kama hizi, kuhudhuria mafunzo na hata semina mbalimbali. Kujua zaidi kuhusu wewe na biashara yako kukua soma; Hii ndio sababu kubwa kwa nini biashara yako haikui.
4. Epuka chuma ulete kwenye biashara yako.
Tatizo jingine kubwa kwenye mafanikio ya biashara zetu ni chuma ulete. Chuma ulete ameturudisha nyuma sana kwenye biashara zetu na wengine wamejikuta wakifunga biashara zao kabisa. Ubaya wa chuma ulete huenda mpaka sasa hujamjua vizuri na hivyo hutoweza kabisa kupambana naye. Nilishaandika kwa kirefu sana kuhusu chuma ulete na jinsi ya kupambana naye. Kusoma jinsi gani unaweza kuepuka chuma ulete bonyeza maandishi haya na kuielewa vizuri dhana ya chuma ulete na jinsi ya kujikomboa wewe na biashara yako jiunge na KISIMA CHA MAARIFA. Kupata maelezo zaidi jinsi ya kujiunga bonyeza hayo maadhishi.
Kukua na kustawi kwa biashara yako ni jambo ambalo linawezekana vizuri sana kama utajua ni wapi unataka kwenda na utafikaje pale. Anza kufanya mambo hayo manne na utaona mabadiliko makubwa sana kwenye biashara zako.
Kwa ushauri zaidi wa kivitendo wa namna ya kuiondoa biashara yako hatua moja mpaka nyingine tafadhali wasiliana na mimi kwa mawasiliano hayo hapo chini.
Nakutakia kila la kheri katika safari hii ya mafanikio

Friday, 1 August 2014

Looking For 100,000$

A SACOOs based in Mbeya city, tanzania is looking for 100,000$ to source Women Entrepreneurs project.
I you would like to contribute or donate please call us at +255 766 46 10 68 or email us on mihingasime@gmail.com or cardinasime@yahoo.com


Saturday, 18 January 2014

wadudu kumbikumbi

Wengi wetu tumekuwa tukisikia kuwa kuna wadudu watamu sana na hupatikana sana hasa katika msimu wa Mvua, wadudu hao ambao ni Maarufu kwa jina la Kumbikumbi huanza kujitokeza wakati wa mvua hasa katika vichuguu vyao vikubwa ambavyo hufaamika kwa kuishi wadudu wengine wanaojulikana kwa jina la mchwa hawa hugeuka na kuja kuwa kumbikumbi. Mkoa wa Mbeya ni moja ya maeneo ambayo kunapatikana kumbikumbi kwa wingi sana . Hiki ni kichuguu ambacho kimefunikwa kwa umahili kabisa.
 

Friday, 3 January 2014

UTALII WA ZIWA NYA



UNATANGAZA UTALII WA NDANI: IFAHAMU HISTORIA YA ZIWA NYASA NA UNDANI WAKE.

Ziwa Nyasa (katika Malawi: Lake Malawi; katika Msumbiji: Niassa) ni kati ya maziwa makubwa ya Afrika ya Mashariki ikiwa na nafasi ya tatu baada ya Viktoria Nyanza na Ziwa Tanganyika.


Lina urefu wa 560 km na upana wa 50-80 km. Vilindi vyake vinaelekea hadi mita 704 chini ya uwiano wa maji yake.
Ziwa Nyasa linapatikana kati ya nchi za Malawi, Msumbiji na Tanzania.Description: https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjahxzZJ_mkg5tPTMN86kVkJYZHQC5Mp_8bsa8B8OzHaxYWKN498TRe5yDU_-QDD37MnZVmLAXSo_3Cvf1pD8LWNotvqYIBIREFzmqGbh4Cyw0Ws4TUkhZfY4OKUzOqnQb3ARvySwV8eQs8/s1600/N1.jpg
 Mwonekano wa Jiwe la kihistoria kwa ubavuni linalojulikana kwa jina Pomonda lililopo Ziwa Nyasa lililotumiwa kujificha na wananchi wakati wa Vita vya Dunia.


 Jiwe la POMONDA likionekana kwa nje katika Ziwa Nyasa eneo la Liuli.
 Kivutio kimoja wapo katika Mwambao wa Ziwa Nyasa katika eneo jirani na Jiwe la Pomonda ni Machweo ya Jua (SUNSITE)kama yanavyoonekana pichani kwa mbali
 Jiwe la POMONDA lililopo katika Ziwa Nyasa hapo ni nje ya Pango ambalo kwa ndani lina uwezo wa kuhifadhi watu 250 kwa wakati mmoja hapo ni namna maji kupwa yanavyoonekana pembeni mwa jiwe hilo.
 Ufukwe wa Ziwa Nyasa namna unavyoonekana pichani na kuvutia kwa Madhari ambapo shughuli za kiuchumi kwa Wananchi wa Ziwa Nyasa huzifanya eneo la Mwambao wa Ziwa Nyasa au kuvuka Nchi jirani ya Malawi ambayo imetenganishwa na Ziwa Nyasa.

 Washiriki wa Mdahalo wa Mabadiliko ya HAli ya Hewa uliofanyika Liuli Wilayani Nyasa kwa Ufadhili wa Foundation for Civil Society wakionyesha Jiwe la POMONDA linalovutia watalii mbalimbali wanaokuja kutembelea Ziwa Nyasa.
 Hapo ni Meli ya MV Songea ambayo hutumika kusafirisha Abiria na Bidhaa kutoka Tanzania kuelekea Malawi kupitia Ziwa Nyasa ikiwa imetia Nanga Liuli Ziwa Nyasa


 Taarifa zilizotolewa na Wazee waishio katika eneo la Mwambao wa Ziwa nyasa wamesema kipimo cha ujazo wa Maji ya Ziwa Nyasa kujua yanapungua au yanaongezeka ni alama hizo zinazoonekana mistari mieupe na rangi nyeusi kuwa ziwa limepungua maji kwa kiasi kikubwa ambapo awali yalifikia katika mistari inayoonekana kwenye jiwe hilo ewa 



Kusini mwa ziwa unatoka Mto Shire unaopeleka maji kwenye Mto Zambezi na hatimaye Bahari Hindi.
Kijiolojia ziwa ni sehemu ya Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki.


Eneo la ziwa ni 29,600 km². Sehemu kubwa ni eneo la Malawi, robo ya kusini-mashariki ni eneo la Msumbiji, robo ya kaskazini-mashariki ni eneo la Tanzania. Lakini kuna ugomvi kati ya Malawi na Tanzania kuhusu mipaka. Malawi imedai ya kwamba maji yote hadi ufukoni upande wa Tanzania ni sehemu ya eneo lake la kitaifa. Tanzania imedai ya kwamba mpaka uwepo katikati kufuatana na uzoefu wa kimataifa.